You are here

Shows

Shows by SOAS Radio

Baada ya mapumziko katika wiki wa uchaguzi hapa SOAS, tumerejea! Tunazungumzia matokeao ya uchaguzi na hukumu iliyotolewa na mahakama ya kimataifa ya jinai ICC.  

Songa ft. Ghetto Ambassador - Mathematrix Abbas Kubaff - Safari na Hii Abbas Salu T - Uzoefu Professor Jay - Zali la Mentali

Wakati wa uchaguzi umewadia! Sikiliza wagombea wakieleza kwa ufupi kampeni zao na 'uchambuzi wa kina' kutoka Bwana Rob na Dada DK.

Joh Makini - Muda
Walanguzi - Mziki wa Kulevya
X Plastaz - Aha!
Bonta - Nauza Kura Yangu

Akili freshi kutoka uzinduzi wa kitabu cha Mtazamo Mbovu wa Somalia? ambacho kimeandikwa na Mary Harper, tunazungumza kuhusu maoni ya kawaida na tofauti yake kulingala na uhalisi. Pia tumefurahi kuwa na Chege Githiora akieleza umuhimu wa lugha za mama.

Fid Q na Doreen - Nyota ya Mchezo

Cool Muza na Montango - Wanangu wa Mtaani

Ndugus - Asali

Nikki Mbishi - Kijusi

Je, unafahamu umuhimu wa redio katika jamii? Siku ya redio duniani huadhumishwa kila mwaka tarehe 13 Februari na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO limetanabaisha umuhimu wa redio kama njia mojawapo ya mawasiliano na hivyo kuandaa siku hiyo maalum. Sema Sasa inaadhimisha Siku ya Redio duniani kwa kuzungumzia umuhimu wa redio katika jamii. Pia tunazungumuzia kongamano la kiswahili mjini Bayreuth Ujerumani, mwaka huu ukiwa ni mwaka wa jubilii kwa kongamano hili, ambalo huandaliwa kama hafla ya kudumisha na kukuza lugha ya Kiswahili.

Hapa SOAS tunaadhimisha siku ya redio duniani. Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu,Sayansi na Utamaduni UNESCO, limetenga tarehe 13 Februari kila mwaka kuwa siku ya redio duniani. Tunazungumuzia umuhimu wa redio katika kudumisha lugha ya kiswahili, pamoja na umuhimu wa redio katika jamii. Sikiliza watangazaji wa Sema Sasa, Rob na Debula, na mwanafunzi wa Kiswahili hapa Uingereza, Beach Bagenal, akitoa maoni yake.

Hapa SOAS tunaadhimisha siku ya redio duniani. Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu,Sayansi na Utamaduni limetenga tarehe 13 Feb kila mwaka kuwa siku ya redio duniani. Tunazungumuzia umuhimu wa redio, ustawishaji wa lugha ya kiswahili kupita redio, pamoja na umuhimu wa redio katika jamii. Sikiliza watangazaji wa Sema Sasa, Rob na Debula, na maoni ya mwanafunzi wa Kiswahili hapa Uingereza, Beach Bagenal.

Kama kawa hapa Sema Sasa. Tunazungumzia msimu wa baridi wa siku hizi, halafu mada muhimu ya kesi ya Wakenya kule Mahakama ya Kimataifa ya Jinai. Bila shaka tunakuleteni nyimbo maarufu za Hip Hop kutoka Afrika Mashariki!

Nyimbo:

Sugu aka Mr. II - Kiburi
ZAiid - Mziki Asili Yake Wapi
Miraba Minne - Vina Mpaka Uchina
Kalamashaka - Constantly

Mwaka mpya mpo? Tumerejea baada ya shamrashamra za Krismasi na kipindi chetu motomoto! Bila shaka muziki wa hip hop, na soga la kuchangamsha bila kusahau habari. Juma hili tunazungumzia shughuli zetu wakati wa Krismasi na matukio duniani! Wasanii wiki hii ni:
X Plastaz - Msimu kwa Msimu
Ndugus - Bila Chuki
Wakazi - Hali Halisi
Fid Q - Ielewe Mitaa

Debula na Bwana Rob wanazungumza na David, mwanafunzi wa muziki mwaka wa pili, juu ya uzoefu wake wa muziki kule Afrika Mashariki, na Jason, aliyeunga mikono kuanzisha chama cha Swahili hapa SOAS juu ya mambo ya Swahili hapa London. Pamoja na maoni kuhusu mgomo wa terehe 30 Novemba, na nyimbo maarufu kutoka Afrika Mashariki, usikose kipindi hiki!

Chiku K Ft. Lameck Ditto - Muda Umefika
Fid Q - Shimo Limetema
Solo Thang - Mambo ya Pwani
RIC - Shikamana

Bila shaka tumerejea! Muziki kemkem pamoja na mgeni maalum kutoka Tanzania! Changamkia miondoko ya Hip Hop kutoka Bongo hadi Nairobi pamoja na mazungumzo na wageni wetu. Wiki hii, tunazumgumzia ukosefu wa ajira hapa Uingereza na wageni wetu wanatujuvya namna ya kutafuta kazi Uingereza na ng'ambo pia. Burudika!

Wiki hii tumerudi na Debula na Bwana Rob wanaokuleteni nyimbo mpya na za kale, pamoja na habari na mambo mpya. Tunajadili maandamano ya wanafunzi na wageni maalum kutoka SOAS na Birkbeck, pia mjue tulifanya nini kwa usiku wa Bonfaya.

Tracks:

ROMA – Tanzania
Sugu – Mikononi mwa Polisi
Ndugus – Niseme
X Plastaz ft Fid Q and Bamba Nazar – Afrika

Katika kipindi cha kwanza cha Sema Sasa tunafurahi kukuletea muziki za Hip-Hop kutoka Tanzania na Kenya na mazungumzo na wageni watatu ambao ni wanafunzi wa SOAS. Tunachukua safari ya muziki, na tutapeleleza ni kwa nini wanafunzi wengi wanataka kusoma Kiswahili siku hizi. Ukitaka kujua, sikiliza!

Nyimbo: Profesor Jay - Nangatuka
Gaza, Ndolo na Johny - I Am
Zaiid - Mwanzo Mwisho